Askofu mstaafu wa Dayosisi ya Kaskazini ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dk. Martin Shao, amefariki dunia leo baada ya kuugua kwa muda mrefu.
Katibu Mkuu wa Dayosisi hiyo, Mhandisi Zebadia Moshi, kupitia taarifa yake aliyoitoa Agosti 25,2025, imeeleza kuwa Askofu Dk. Shao, amefariki dunia akiwa katika Hospitali ya Rufani ya Kanda ya KCMC, alikokuwa akipatiwa matibabu.
Dk. Martin Shao, alikuwa Askofu wa awamu ya tatu wa Dayosisi hiyo ya Kaskazini, tangu mwaka 2004 alipochaguliwa kumrithi mtangulizi wake, Askofu Dk. Erasto Kweka (sasa marehemu).
Alitunukiwa shahada ya heshima ya udaktari wa falsafa (PhD), na Chuo Kikuu cha Midland Lutheran College of Nebraska, USA kutokana na uongozi wake uliotukuka na utumishi wa muda mrefu katika huduma za dini.