October 23, 2024

Year: 2024

Mradi wa Ubunifu wa FUNGUO unaotekelezwa na UNDP hapa Tanzania kwa ufadhili wa na Umoja wa Ulaya na mfuko waIMBEJU wa CRDB Bank Foundation, imeamua kushirikiana ili kubadilisha mwenendo wa ufadhili wa wajasiriamali wabunifuhapa nchini. Ushirikiano huu wa kimkakati unalenga kutumiaruzuku inayotolewa na Umoja wa Ulaya kwa kampuni changa nakufungua fursa ya kupata mikopo ya riba na masharti nafuukutoka kwa CRDB Bank Foundation, ili kuongeza uwezo wakimtaji kuwawezesha wajasiriamali kukua kwa haraka zaidi. Tangu kuanziswa kwake mwaka 2022 kwa ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya kupitia mpango wa BEGIN unaoratibiwa na kitengacha mazingira ya biashara katika Ofisi ya Rais – Mipango naUwezeshaji, FUNGUO  imewekeza zaidi ya TZS bilioni 3.8 katika kampuni changa 43, ikichangia  katika kutengeneza nakuendeleza takribani ajira 4000 za moja kwa moja na zisizo za moja kwa  kwa vijana wa Tanzania. Dhamira ya mpango huu nikuongeza idadi ya kampuni za ubunifu zenye uwezo wa kustawiharaka ili kuharakisha kufikia Malengo ya Maendeleo Endelevuya Tanzania. Wafadhili wengine wa mradi wa FUNGUO nipamoja na Serikali ya Uingereza kupitia mpango wa Africa Technology and Innovation Partnerships (ATIP) na UNDP katikamkakati wake wa kuwawezesha vijana kiuchumi. Mwaka huu, FUNGUO imepanga kutoa hadi TZS bilioni 1.4, ikilenga kwa makusudi kuwawezesha  wanawake walioanzishabiashara zenye ubunifu ndani yake....