Polisi nchini Somalia wamesema watu tisa wameuawa kwenye shambulio lililofanywa na wapiganaji wa kundi la Al Shabaab katika hoteli maarufu ya Pearl iliyo ufukweni jijini Mogadishu.
Kundi hilo la Al shabaab limekiri kuhusika na shambulio hilo kwenye hotel maarufu ya Pearl katika fukwe za mji mkuu wa Somalia, Mogadishu.
Miongoni mwa waliouawa katika hoteli hiyo maarufu ínayoitwa Pearl, ni raia sita na askari watatu, polisi wameeleza katika taarifa yao.